Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mzee Philip Mangula akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Iringa Vijijini Mama Delfina Mtavilalu mara baada ya kuw...
Akizungumza na waandishi wa habari huku akionyesha moja ya gazeti lililowahi kuripoti kampeni hizo kwa picha Philip Mangula amelaani kampeni alizodai zinadhalilisha watoto zinazofanywa na CHADEMA huku akionyesha mmoja wa watoto ambaye alipigwa picha huku akionyesha sare zake za shule ambazo zimechakaa na kuchanika na mmoja wa wapiga debe wa chama hicho akisema kutangaza umasikini wa mtu ni kumdhalilisha
Philip Mangula akiingia katika ofisi za mkoa wa Iringa huku akiwa ameongozana na Katibu wa Mkoa wa Iringa Bw. Hassan Mtenga na viongozi wengine.
Kipande Cha Gazeti hilo kikionyesha picha iliyochapishwa hivi karibuni inayodaiwa kumdhalilisha mtoto.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mzee Philip Mangula akielezea zaidi kuhusu picha hiyo
Mwandishi wa habari wa ITV Bw. Silvanus Kigomba akiuliza swali kwa Mzee Philip Mangula wakati wa mkutano huo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mzee Philip Mangula akifafanua zaidi swali la mwandishi huyo
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mzee Philip Mangula akielezea mambo mbalimbali yanayohusu uchaguzi huo ambapo amesema CCM ni waumini wa Amani na kwamba katika jimbo la Kalenga hagombei Godfrey Mgimwa bali kinachogombea ni Chama cha Mapinduzi kwani ungekuwa ni ukoo wa mgimwa unagombea basi ungeona akina mgimwa woote wako mbelea wakipiga debe ili washinde lakini kwa sababu ni CCM inagombea ndiyo maana utaona viongozi na wana CCM mbalimbali wakishiriki katika kampeni hizo ili kukipatia ushindi chama chao.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mzee Philip Mangula akizungumza nabaadhi ya viongozi wa CCM mkoa wa Iringa kabla ya kuelekea Ifunda ambako atapiga kambi huko.